-
2 Samweli 5:22-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Baadaye Wafilisti wakaja tena na kuenea katika Bonde la* Refaimu.+ 23 Daudi akamwomba Yehova ushauri, lakini Akasema: “Usipande moja kwa moja. Badala yake, zunguka nyuma yao, uwashambulie mbele ya vichaka vya mibaka. 24 Na utakaposikia sauti ya watu wakipiga mwendo juu ya vichaka vya mibaka, tenda bila kusita, kwa sababu mimi Yehova nitakuwa nimetangulia mbele yako kuliua jeshi la Wafilisti.” 25 Basi Daudi akafanya kama Yehova alivyomwamuru, akawaua Wafilisti+ kuanzia Geba+ mpaka Gezeri.+
-