-
2 Samweli 10:9-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Yoabu alipoona kwamba anashambuliwa upande wa mbele na wa nyuma, akachagua baadhi ya wanajeshi bora katika Israeli na kuwapanga kivita ili wapigane na Wasiria.+ 10 Wanaume waliobaki aliwaweka chini ya usimamizi wa* Abishai ndugu yake,+ ili awapange kivita kupigana na Waamoni.+ 11 Kisha akasema: “Ikiwa Wasiria watanizidi nguvu, basi mtaniokoa; lakini Waamoni wakiwazidi ninyi nguvu, nitawaokoa. 12 Ni lazima tuwe imara na jasiri+ kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya majiji ya Mungu wetu, naye Yehova atafanya yaliyo mema machoni pake.”+
-