-
2 Samweli 24:10-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Lakini moyo wa Daudi ukajaa* majuto+ baada ya kuwahesabu watu. Basi Daudi akamwambia Yehova: “Nimetenda dhambi+ kubwa kwa kufanya jambo hili. Na sasa, Yehova, tafadhali nisamehe kosa langu mimi mtumishi wako,+ kwa maana nimetenda kwa upumbavu sana.”+ 11 Daudi alipoamka asubuhi, neno la Yehova likamjia nabii Gadi,+ mwonaji wa Daudi, likisema: 12 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakupa mambo matatu ya kuchagua. Chagua jambo nitakalokutendea.”’”+ 13 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia: “Je, unataka njaa kali ije katika nchi yako kwa miaka saba?+ Au unataka kuwakimbia maadui wako kwa miezi mitatu huku wakikufuatia? + Au unataka nchi yako ikumbwe na ugonjwa hatari kwa siku tatu?+ Sasa fikiria kwa makini jibu ninalopaswa kumpa Yule aliyenituma.” 14 Kwa hiyo Daudi akamwambia Gadi: “Jambo hilo linanihuzunisha sana. Tafadhali, acha tuanguke mkononi mwa Yehova,+ kwa maana rehema zake ni nyingi;+ lakini usiniache nianguke mkononi mwa mwanadamu.”+
-