-
2 Samweli 24:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Ndipo Yehova akaleta ugonjwa hatari+ Israeli kuanzia asubuhi mpaka wakati uliowekwa, hivi kwamba watu 70,000 wakafa+ kuanzia Dani mpaka Beer-sheba.+ 16 Malaika alipounyoosha mkono wake kuelekea jiji la Yerusalemu ili kuliangamiza, Yehova akaghairi* kwa sababu ya msiba huo,+ akamwambia malaika aliyekuwa akiwaangamiza watu: “Imetosha! Sasa shusha mkono wako.” Malaika wa Yehova alikuwa karibu na uwanja wa kupuria nafaka wa Arauna+ Myebusi.+
-