-
Mwanzo 49:8-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 “Nawe Yuda,+ ndugu zako watakusifu.+ Mkono wako utakuwa shingoni mwa maadui wako.+ Wana wa baba yako watainama chini mbele yako.+ 9 Yuda ni mwanasimba.+ Mwanangu, kwa hakika utapanda juu kutoka mawindoni. Amejikunyata chini na kujinyoosha kama simba, na kama simba, ni nani anayethubutu kumwamsha? 10 Fimbo ya ufalme haitaondoka Yuda,+ wala fimbo ya kiongozi kutoka katikati ya miguu yake, mpaka Shilo* atakapokuja,+ na mataifa yatamtii.+ 11 Atamfunga punda wake kwenye mzabibu na mwanapunda dume wake kwenye mzabibu bora, naye atafua nguo zake katika divai na vazi lake katika damu ya zabibu. 12 Macho yake ni mekundu sana kwa sababu ya divai, na meno yake ni meupe kwa sababu ya maziwa.
-