Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 7:51
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 51 Kwa hiyo Mfalme Sulemani akakamilisha kazi yote aliyopaswa kufanya kwa ajili ya nyumba ya Yehova. Kisha Sulemani akaingiza ndani vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa amevifanya kuwa vitakatifu,+ naye akaweka fedha, dhahabu, na vitu hivyo katika hazina za nyumba ya Yehova.+

  • 1 Wafalme 14:25, 26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Katika mwaka wa tano wa Mfalme Rehoboamu, Mfalme Shishaki+ wa Misri alishambulia Yerusalemu.+ 26 Akachukua hazina za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mfalme.*+ Alichukua kila kitu, kutia ndani ngao zote za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Kulikuwa na walinzi wakuu* wanne waliowekwa katika wadhifa huo wa kuaminiwa. Walikuwa Walawi, nao walisimamia vyumba* na hazina za nyumba ya Mungu wa kweli.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 18:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 mara moja alimtuma Hadoramu mwana wake kwa Mfalme Daudi ili amjulie hali na kumpongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda (kwa maana mara nyingi Hadadezeri alimshambulia Tou), na Hadoramu alimletea Daudi kila aina ya vitu vya dhahabu, fedha, na shaba. 11 Mfalme Daudi akavitakasa vitu hivyo ili viwe vya Yehova,+ pamoja na fedha na dhahabu aliyokuwa amechukua kutoka kwa mataifa yote: kutoka kwa Waedomu na Wamoabu, kutoka kwa Waamoni,+ Wafilisti,+ na Waamaleki.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki