-
1 Wafalme 11:29-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 Wakati huo Yeroboamu alitoka Yerusalemu, na nabii Ahiya,+ Mshilo, akamkuta njiani. Ahiya alikuwa amevaa nguo mpya, na wote wawili walikuwa peke yao shambani. 30 Ahiya akashika nguo mpya aliyokuwa amevaa na kuirarua vipande 12. 31 Kisha akamwambia Yeroboamu:
“Jichukulie vipande kumi, kwa maana Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Tazama, ninaurarua ufalme kutoka mikononi mwa Sulemani, nami nitakupa makabila kumi.+
-