-
1 Wafalme 22:42, 43Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka 35 alipowekwa kuwa mfalme, naye alitawala kwa miaka 25 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Azuba binti ya Shilhi. 43 Yehoshafati aliendelea kutembea katika njia yote ya Asa+ baba yake. Hakugeuka na kuiacha njia hiyo, naye alitenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova.+ Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa, na bado watu walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu.+
-