Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 14:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Na watu wa Yuda walikuwa wakitenda maovu machoni pa Yehova,+ na kwa dhambi zao walimkasirisha kuliko walivyofanya mababu zao.+ 23 Pia waliendelea kujijengea mahali pa juu, nguzo takatifu, na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu+ na chini ya kila mti wenye majani mengi.+

  • 2 Wafalme 15:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu+ mwana wa Mfalme Uzia+ wa Yuda akawa mfalme.

  • 2 Wafalme 15:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa, na watu bado walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu.+ Yeye ndiye aliyejenga lango la juu la nyumba ya Yehova.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 21:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka 32 alipoanza kutawala, naye alitawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 21:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Alikuwa amejenga pia mahali pa juu+ kwenye milima ya Yuda, akasababisha wakaaji wa Yerusalemu wafanye ukahaba wa kiroho, naye akawapotosha watu wa Yuda.

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 55 huko Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Alijenga upya mahali pa juu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amebomoa,+ akajenga madhabahu kwa ajili ya Mabaali na kutengeneza miti mitakatifu,* naye akaliinamia jeshi lote la mbinguni na kuliabudu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki