-
1 Wafalme 7:40-46Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
40 Hiramu+ alitengeneza pia mabeseni, sepetu,+ na mabakuli.+ Basi Hiramu akamaliza kazi yote aliyomfanyia Mfalme Sulemani kuhusiana na nyumba ya Yehova:+ 41 zile nguzo mbili+ na vifuniko vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; na nyavu mbili+ za kufunika vifuniko hivyo viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; 42 yale makomamanga 400+ kwa ajili ya zile nyavu mbili, safu mbili za makomamanga kwa ajili ya kila wavu, ili kufunika vile vifuniko viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya zile nguzo mbili; 43 yale magari kumi+ na yale mabeseni kumi+ yaliyokuwa juu ya magari hayo; 44 ile Bahari+ na wale ng’ombe dume 12 waliokuwa chini ya Bahari hiyo; 45 na ndoo za kuondolea majivu, sepetu, mabakuli, na vyombo vyote ambavyo Hiramu alimtengenezea Mfalme Sulemani kwa shaba iliyong’arishwa kwa ajili ya nyumba ya Yehova. 46 Mfalme alivitengeneza katika kalibu za udongo wa mfinyanzi katika wilaya ya Yordani, kati ya Sukothi na Sarethani.
-