10 Kisha kuhani Ezra akasimama na kuwaambia: “Mmetenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa kuoa wanawake wa kigeni+ na hivyo mmeongeza hatia ya Israeli. 11 Sasa ungameni kwa Yehova Mungu wa mababu zenu na mfanye mapenzi yake. Jitengeni na watu wa mataifa na hawa wake wa kigeni.”+
9Siku ya 24 ya mwezi huo, Waisraeli wakakusanyika; walikuwa wamefunga wakiwa wamevaa nguo za magunia na kujirushia mavumbi.+2 Kisha wazao wa Waisraeli wakajitenga na wageni wote,+ wakasimama na kuungama dhambi zao wenyewe na makosa ya baba zao.+