Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 139:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Nikisema: “Hakika giza litanificha!”

      Basi usiku unaonizunguka utakuwa nuru.

      12 Hata giza halitakuwa zito mno kwako,

      Lakini usiku utakuwa mwangavu kama mchana;+

      Kwako giza ni sawa na nuru.+

  • Isaya 29:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ole wao wanaojitahidi sana kumficha Yehova mipango yao.*+

      Wanatenda matendo yao mahali penye giza,

      Huku wakisema: “Ni nani anayetuona?

      Ni nani anayejua kutuhusu?”+

  • Yeremia 23:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 “Je, mtu yeyote anaweza kujificha mahali pa siri ambapo siwezi kumwona?”+ auliza Yehova.

      “Je, mimi sizijazi mbingu na dunia?”+ auliza Yehova.

  • Amosi 9:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Nao wakijificha kwenye kilele cha Karmeli,

      Nitawasaka na kuwatoa huko.+

      Wakijificha chini ya bahari ili macho yangu yasiwaone,

      Huko nitamwamuru nyoka awaume.

  • Waebrania 4:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Na hakuna kiumbe kilichofichwa machoni pake,+ bali vitu vyote viko uchi navyo vimefunuliwa wazi machoni pa yule ambaye tunapaswa kutoa hesabu kwake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki