-
2 Wafalme 24:11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alikuja wakati watumishi wake walipokuwa wakilizingira jiji hilo.
-
-
Yeremia 28:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
28 Mwaka huohuo, mwanzoni mwa utawala wa Mfalme Sedekia+ wa Yuda, katika mwaka wa nne, mwezi wa tano, nabii Hanania mwana wa Azuri kutoka Gibeoni+ aliniambia hivi katika nyumba ya Yehova mbele ya makuhani na watu wote: 2 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi, ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babiloni.+ 3 Katika muda wa miaka miwili* nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Yehova ambavyo Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alivichukua mahali hapa na kuvipeleka Babiloni.’”+
-
-
Danieli 1:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Yehoyakimu+ wa Yuda, Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alikuja na kuzingira Yerusalemu.+ 2 Baada ya muda Yehova akamtia Mfalme Yehoyakimu wa Yuda mikononi mwake,+ pamoja na baadhi ya vyombo vya nyumba ya* Mungu wa kweli, akavileta katika nchi ya Shinari*+ katika nyumba ya* mungu wake. Akaviweka katika hazina ya mungu wake.+
-