Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 23:31-34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Yehoahazi+ alikuwa na umri wa miaka 23 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miezi mitatu huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 32 Yehoahazi alianza kutenda maovu machoni pa Yehova, alitenda mambo yote ambayo mababu zake walitenda.+ 33 Farao Neko+ alimtia gerezani kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi, ili kumzuia asitawale Yerusalemu, kisha akaitoza nchi faini ya talanta 100 za fedha* na talanta moja ya dhahabu.+ 34 Isitoshe, Farao Neko alimweka Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme baada ya Yosia baba yake na kubadili jina lake kuwa Yehoyakimu; lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri,+ ambako alifia hatimaye.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Zaidi ya hayo, mfalme wa Misri alimweka Eliakimu ndugu ya Yehoahazi kuwa mfalme wa Yuda na Yerusalemu na kubadili jina lake kuwa Yehoyakimu; lakini Neko+ akamchukua Yehoahazi ndugu yake na kumpeleka Misri.+

  • Yeremia 22:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Kwa maana Yehova anasema hivi kumhusu Shalumu*+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda anayetawala badala ya Yosia+ baba yake, ambaye ameondoka mahali hapa: ‘Hatarudi hapo tena. 12 Kwa maana atakufa mahali walipompeleka uhamishoni, naye hataiona tena nchi hii.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki