-
2 Wafalme 23:31-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Yehoahazi+ alikuwa na umri wa miaka 23 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miezi mitatu huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 32 Yehoahazi alianza kutenda maovu machoni pa Yehova, alitenda mambo yote ambayo mababu zake walitenda.+ 33 Farao Neko+ alimtia gerezani kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi, ili kumzuia asitawale Yerusalemu, kisha akaitoza nchi faini ya talanta 100 za fedha* na talanta moja ya dhahabu.+ 34 Isitoshe, Farao Neko alimweka Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme baada ya Yosia baba yake na kubadili jina lake kuwa Yehoyakimu; lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri,+ ambako alifia hatimaye.+
-