-
Yeremia 3:6-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Katika siku za mfalme Yosia,+ Yehova aliniambia: “‘Je, umeona mambo ambayo Israeli asiye mwaminifu ametenda? Amepanda juu ya kila mlima mrefu na kwenda chini ya kila mti wenye majani mengi ili afanye ukahaba.+ 7 Hata baada ya kufanya mambo hayo yote, niliendelea kumwambia arudi kwangu,+ lakini hakurudi; na Yuda akaendelea kumtazama dada yake mwenye hila.+ 8 Nilipoona hivyo, nikamfukuza Israeli asiye mwaminifu akiwa na cheti kamili cha talaka+ kwa sababu ya uzinzi wake.+ Lakini Yuda dada yake mwenye hila hakuogopa; yeye pia alienda na kufanya ukahaba.+
-
-
Ezekieli 16:46, 47Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
46 “‘Dada yako mkubwa ni Samaria,+ anayekaa upande wako wa kaskazini* pamoja na mabinti zake,*+ na dada yako mdogo, anayekaa upande wako wa kusini,* ni Sodoma+ pamoja na mabinti zake.+ 47 Hukutembea tu katika njia zao na kufuata mazoea yao yanayochukiza, bali pia kwa muda mfupi mwenendo wako ulikuwa mpotovu hata zaidi kuliko mwenendo wao.+
-