Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 6:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Yehova Mungu wenu atakapowaleta katika nchi aliyowaapia mababu zenu Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwamba atawapa ninyi+—majiji makubwa na yenye kupendeza ambayo hamkujenga,+ 11 nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina mbalimbali ambavyo hamkufanya kazi ili kuvipata, visima ambavyo hamkuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hamkupanda—nanyi mtakapokuwa mmekula na kushiba,+ 12 jihadharini msimsahau Yehova,+ aliyewatoa nchini Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.

  • Kumbukumbu la Torati 8:12-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Baada ya kula na kushiba na kujenga nyumba nzuri na kukaa humo,+ 13 ng’ombe wenu na kondoo wenu watakapokuwa wameongezeka na fedha yenu na dhahabu yenu itakapokuwa imeongezeka na mtakapokuwa na wingi wa vitu vyote, 14 msiache mioyo yenu iwe na kiburi+ na kuwafanya mumsahau Yehova Mungu wenu, aliyewatoa nchini Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa,+

  • Kumbukumbu la Torati 32:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Yeshuruni* aliponenepa, alipiga teke kwa uasi.

      Umenenepa, una mafuta mengi mwilini, tumbo lako limenenepa.+

      Basi akamwacha Mungu, aliyemuumba,+

      Na kumdharau Mwamba wa wokovu wake.

  • Kumbukumbu la Torati 32:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Mlimsahau Mwamba,+ baba yenu aliyewazaa,

      Nanyi hamkumkumbuka Mungu aliyewazaa.+

  • Isaya 17:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana umemsahau Mungu+ wa wokovu wako;

      Hukumkumbuka Mwamba+ wa ngome yako.

      Ndiyo sababu unapanda mashamba makubwa maridadi*

      Na kupanda humo chipukizi la mgeni.*

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki