-
2 Mambo ya Nyakati 7:6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Makuhani walikuwa wamesimama katika vituo vyao vya kazi, na Walawi pia waliokuwa na ala za muziki zilizopigwa kuambatana na nyimbo ambazo Yehova aliimbiwa.+ (Mfalme Daudi alikuwa ametengeneza ala hizo ili kumshukuru Yehova—“kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele”—wakati Daudi alipokuwa akitoa sifa pamoja nao.*) Na makuhani walikuwa wakipiga tarumbeta kwa sauti kubwa+ mbele yao, huku Waisraeli wote wakiwa wamesimama.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 29:25, 26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Wakati huo, aliwaweka Walawi katika nyumba ya Yehova wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi,+ kulingana na amri ya Daudi+ na ya Gadi+ mwonaji wa mfalme na ya nabii Nathani,+ kwa maana amri hiyo ilitoka kwa Yehova kupitia manabii wake. 26 Basi Walawi walikuwa wakisimama wakiwa na ala za Daudi, na makuhani wakiwa na tarumbeta.+
-