-
Hesabu 6:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 anapaswa kujiepusha na divai na vinywaji vingine vyenye kileo. Hapaswi kunywa siki ya divai au siki ya kitu chochote chenye kileo.+ Hapaswi kamwe kunywa maji ya zabibu, wala kula zabibu zilizotoka kuchumwa au zilizokaushwa. 4 Siku zote atakazokuwa Mnadhiri hapaswi kula kitu chochote kinachotokana na mzabibu, kuanzia zabibu ambazo hazijaiva mpaka maganda yake.
-