17 “Na lazima Edomu awe kitu cha kutisha.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa hofu na kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote. 18 Kama Sodoma na Gomora na miji jirani ilivyoangamizwa,”+ Yehova anasema, “hakuna mtu atakayekaa huko, na hakuna mtu atakayeishi huko.+
15 Kama ulivyoshangilia urithi wa watu wa nyumba ya Israeli ulipofanywa ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea.+ Utakuwa magofu yaliyo ukiwa, ewe eneo lenye milima la Seiri, naam, Edomu yote;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”