Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 50:8-15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Siwakaripii kwa sababu ya dhabihu zenu,

      Wala kwa sababu ya dhabihu zenu nzima za kuteketezwa ambazo daima ziko mbele zangu.+

       9 Sihitaji kuchukua ng’ombe dume katika nyumba yako,

      Wala mbuzi* katika mazizi yako.+

      10 Kwa maana kila mnyama wa mwituni ni wangu,+

      Hata wanyama walio juu ya milima elfu moja.

      11 Ninamjua kila ndege wa milimani;+

      Wanyama wasio na idadi wa mbugani ni wangu.

      12 Ningekuwa na njaa, nisingekwambia,

      Kwa maana nchi inayozaa na kila kitu kilichomo ni changu.+

      13 Je, nitakula nyama ya ng’ombe dume

      Na kunywa damu ya mbuzi?+

      14 Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+

      Na utimize nadhiri zako kwa Aliye Juu Zaidi;+

      15 Nililie wakati wa taabu.+

      Nitakuokoa, nawe utanitukuza.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki