8 Siwakaripii kwa sababu ya dhabihu zenu,
Wala kwa sababu ya dhabihu zenu nzima za kuteketezwa ambazo daima ziko mbele zangu.+
9 Sihitaji kuchukua ng’ombe dume katika nyumba yako,
Wala mbuzi katika mazizi yako.+
10 Kwa maana kila mnyama wa mwituni ni wangu,+
Hata wanyama walio juu ya milima elfu moja.
11 Ninamjua kila ndege wa milimani;+
Wanyama wasio na idadi wa mbugani ni wangu.
12 Ningekuwa na njaa, nisingekwambia,
Kwa maana nchi inayozaa na kila kitu kilichomo ni changu.+
13 Je, nitakula nyama ya ng’ombe dume
Na kunywa damu ya mbuzi?+
14 Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+
Na utimize nadhiri zako kwa Aliye Juu Zaidi;+
15 Nililie wakati wa taabu.+
Nitakuokoa, nawe utanitukuza.”+