-
Kumbukumbu la Torati 31:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Wakati huo hasira yangu itawaka dhidi yao,+ nami nitawaacha+ na kuuficha uso wangu wasiuone+ mpaka watakapoangamia. Kisha baada ya kupatwa na misiba na mateso mengi,+ watasema, ‘Je, hatujapatwa na misiba hii kwa sababu Mungu wetu hayuko miongoni mwetu?’+ 18 Lakini nitaendelea kuuficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yote waliyotenda kwa kuigeukia miungu mingine.+
-
-
Isaya 3:11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Ole wake mtu mwovu!
Atapatwa na msiba,
Atatendewa yale ambayo mikono yake imetenda!
-