-
Yoshua 6:18, 19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Lakini mjiepushe na kitu chochote kinachopaswa kuharibiwa,+ ili msikitamani kitu kinachopaswa kuharibiwa na kukichukua,+ msije mkaleta msiba* kwenye kambi ya Waisraeli.+ 19 Lakini fedha yote na dhahabu na vitu vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Yehova.+ Vinapaswa kupelekwa katika hazina ya Yehova.”+
-
-
Isaya 23:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Mwishoni mwa miaka 70, Yehova atalikazia fikira Tiro, nalo litarudia malipo yake na kufanya ukahaba na falme zote za ulimwengu zilizo duniani. 18 Lakini faida yake na malipo yake yatakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova. Hayatahifadhiwa wala kuwekwa akiba, kwa sababu malipo yake yatakuwa kwa ajili ya wale wanaokaa mbele za Yehova, ili wale na kushiba na kuvaa mavazi ya kifahari.+
-