Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 7:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Mtu yeyote akigusa kitu chochote kisicho safi, iwe ni uchafu wa mwanadamu+ au mnyama asiye safi+ au kitu chochote chenye kuchukiza kisicho safi,+ kisha ale nyama ya dhabihu ya ushirika, ambayo ni ya Yehova, ni lazima auawe.’”

  • Hesabu 5:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Waamuru Waisraeli wamtoe nje ya kambi kila mtu mwenye ukoma+ na kila mtu anayetokwa na umajimaji+ na kila mtu aliyejichafua kwa kumgusa mtu aliyekufa.*+ 3 Mnapaswa kumtoa nje awe ni mwanamume au mwanamke. Mnapaswa kuwatoa nje ya kambi watu hao ili wasichafue+ kambi za wale ninaokaa* kati yao.”+

  • Hesabu 9:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Sasa watu fulani hawakuwa safi kwa sababu waligusa mtu aliyekufa,+ hivyo hawangeweza kuitayarisha dhabihu ya Pasaka siku hiyo. Kwa hiyo wakaenda kumwona Musa na Haruni siku hiyo,+

  • Hesabu 19:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Mtu yeyote anayemgusa mtu aliyekufa* hatakuwa safi kwa siku saba.+

  • Hesabu 31:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Nanyi mnapaswa kupiga kambi nje ya kambi kwa siku saba. Kila mtu miongoni mwenu ambaye amemuua mtu na kila mtu ambaye amemgusa mtu aliyeuawa+ anapaswa kujitakasa+ siku ya tatu na siku ya saba, ninyi na mateka wenu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki