-
Luka 11:9-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Basi ninawaambia, endeleeni kuomba,+ nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa.+ 10 Kwa maana kila mtu anayeomba hupokea,+ na kila mtu anayetafuta hupata, na kila mtu anayepiga hodi atafunguliwa. 11 Kwa kweli, ni baba gani kati yenu ambaye mwana wake akiomba samaki, atampa nyoka?+ 12 Au pia akiomba yai, atampa nge? 13 Kwa hiyo, ingawa ninyi ni waovu, mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomwomba!”+
-