-
Marko 14:32-36Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
32 Basi wakafika mahali panapoitwa Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake: “Ketini hapa ninaposali.”+ 33 Akaondoka pamoja na Petro, Yakobo, na Yohana,+ naye akaanza kufadhaika* na kutaabika sana. 34 Akawaambia: “Nimehuzunika* sana,+ kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mwendelee kukesha.”+ 35 Akasonga mbele kidogo, akaanguka chini na kuanza kusali kwamba ikiwezekana, saa hiyo ipitilie mbali kutoka kwake. 36 Naye akasema: “Abba,* Baba,+ mambo yote yanawezekana kwako; niondolee kikombe hiki. Lakini si kama ninavyotaka, bali unavyotaka.”+
-