-
Mathayo 15:3-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Akawajibu: “Kwa nini ninyi pia huvunja amri ya Mungu kwa sababu ya mapokeo yenu?+ 4 Kwa mfano, Mungu alisema, ‘Mheshimu baba yako na mama yako,’+ na, ‘Yeyote anayemtukana* baba yake au mama yake anapaswa kuuawa.’+ 5 Lakini ninyi mnasema, ‘Yeyote anayemwambia baba yake au mama yake: “Chochote nilicho nacho ambacho kingekusaidia ni zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu,”+ 6 anakosa kabisa kumheshimu baba yake.’ Kwa hiyo, mmelibatilisha neno la Mungu kwa sababu ya mapokeo yenu.+
-