-
Kutoka 12:14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 “‘Siku hiyo itakuwa ukumbusho kwenu, nanyi mnapaswa kuisherehekea ikiwa sherehe kwa Yehova katika vizazi vyenu vyote. Kwa kuwa ni sheria ya kudumu, mnapaswa kuisherehekea.
-
-
Kumbukumbu la Torati 16:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 “Adhimisheni mwezi wa Abibu* na msherehekee Pasaka ya Yehova Mungu wenu,+ kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Yehova Mungu wenu aliwatoa nchini Misri wakati wa usiku.+ 2 Nanyi mnapaswa kumtolea Yehova Mungu wenu dhabihu ya Pasaka+ kutoka katika kondoo wenu na ng’ombe wenu,+ mahali ambapo Yehova atachagua jina lake likae hapo.+
-