-
Matendo 10:17-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Petro akiwa bado anashangaa kuhusu maana ya maono hayo, wakati huohuo wale watu waliotumwa na Kornelio waliulizia nyumba ya Simoni nao walikuwa wamesimama langoni.+ 18 Nao wakaita kwa sauti na kuuliza ikiwa Simoni anayeitwa Petro alikuwa mgeni humo. 19 Petro alipokuwa akiwaza kuhusu yale maono, roho+ ikasema: “Tazama! Wanaume watatu wanakutafuta. 20 Basi simama, ushuke na kwenda pamoja nao, usiwe na shaka kamwe, kwa sababu nimewatuma.”
-