-
Mwanzo 24:2, 3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Abrahamu akamwambia mtumishi wake, aliyekuwa na umri mkubwa zaidi nyumbani mwake, ambaye alisimamia mali zake zote:+ “Tafadhali, weka mkono wako chini ya paja langu, 3 nami nitakuapisha kwa jina la Yehova, Mungu wa mbingu na Mungu wa dunia, kwamba hutamchukulia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, ninaoishi miongoni mwao.+
-
-
Nehemia 13:25, 26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Ndipo nikawakemea na kuwalaani, nikawapiga baadhi ya wanaume hao,+ nikazing’oa nywele zao na kuwaapisha hivi kwa Mungu: “Msikubali mabinti wenu waolewe na wana wao, na msikubali mabinti wao waolewe na wana wenu au ninyi wenyewe.+ 26 Je, Mfalme Sulemani wa Israeli hakutenda dhambi kwa sababu yao? Hakukuwa na mfalme kama yeye miongoni mwa mataifa mengi;+ naye alipendwa na Mungu wake,+ hivi kwamba Mungu akamweka kuwa mfalme wa nchi yote ya Israeli. Lakini wake wa kigeni walimfanya hata yeye atende dhambi.+
-