Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 24:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Abrahamu akamwambia mtumishi wake, aliyekuwa na umri mkubwa zaidi nyumbani mwake, ambaye alisimamia mali zake zote:+ “Tafadhali, weka mkono wako chini ya paja langu, 3 nami nitakuapisha kwa jina la Yehova, Mungu wa mbingu na Mungu wa dunia, kwamba hutamchukulia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, ninaoishi miongoni mwao.+

  • Kumbukumbu la Torati 7:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Msioane nao kamwe. Msikubali mabinti wenu waolewe na wana wao wala msikubali wana wenu wawaoe mabinti wao.+ 4 Kwa maana watawapotosha wana wenu waache kumfuata Mungu na kuanza kuabudu miungu mingine;+ kisha hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu, naye atawaangamiza upesi.+

  • Nehemia 13:25, 26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Ndipo nikawakemea na kuwalaani, nikawapiga baadhi ya wanaume hao,+ nikazing’oa nywele zao na kuwaapisha hivi kwa Mungu: “Msikubali mabinti wenu waolewe na wana wao, na msikubali mabinti wao waolewe na wana wenu au ninyi wenyewe.+ 26 Je, Mfalme Sulemani wa Israeli hakutenda dhambi kwa sababu yao? Hakukuwa na mfalme kama yeye miongoni mwa mataifa mengi;+ naye alipendwa na Mungu wake,+ hivi kwamba Mungu akamweka kuwa mfalme wa nchi yote ya Israeli. Lakini wake wa kigeni walimfanya hata yeye atende dhambi.+

  • 2 Wakorintho 6:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Msifungwe nira* isivyo sawa pamoja na wasio waamini.+ Kwa maana kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi sheria?+ Au nuru ina ushirika gani na giza?+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki