-
Luka 18:10-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 “Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja alikuwa Farisayo na mwingine mkusanya kodi. 11 Yule Farisayo akasimama na kuanza kusali akisema moyoni, ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wengine—wanyang’anyi, wasio waadilifu, wazinzi—au hata kama mkusanya kodi huyu. 12 Mimi hufunga mara mbili kwa juma; ninatoa sehemu ya kumi ya mapato yangu yote.’+ 13 Lakini yule mkusanya kodi alikuwa amesimama mbali kidogo na hata hakutaka kutazama mbinguni, bali alijipigapiga kifuani akisema, ‘Ee Mungu, nihurumie* mimi mtenda dhambi.’+ 14 Ninawaambia, mtu huyu alishuka kwenda nyumbani akiwa mwadilifu mbele za Mungu kuliko yule Farisayo.+ Kwa sababu kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, lakini yeyote anayejinyenyekeza atainuliwa.”+
-