16 Kwa hiyo, msimruhusu mtu yeyote awahukumu kuhusu mnachokula na kunywa+ au kuhusu kushika sherehe au mwezi mpya+ au sabato.+17 Mambo hayo ni kivuli cha mambo yanayokuja,+ bali uhalisi ni wa Kristo.+
5 Watu hao hufanya utumishi mtakatifu kwa mfano wa uhalisi na kivuli+ cha vitu vya mbinguni;+ kama vile Musa, alipokuwa karibu kujenga hema, alipewa amri na Mungu: Kwa kuwa Mungu anasema: “Hakikisha kwamba unatengeneza vitu vyote kwa kufuata kielelezo ulichoonyeshwa mlimani.”+
10Kwa kuwa Sheria ina kivuli+ cha mambo mema yatakayokuja,+ lakini si uhalisi wa mambo hayo, haiwezi* kamwe kwa dhabihu zilezile zinazotolewa mwaka baada ya mwaka, kuwafanya wale wanaokaribia wawe wakamilifu.+