“Hakuna Kujifunza Biblia kwa Kweli Wakati Wo Wote”
◆ Dr. L. M. Muntingh, mkuu wa idara ya ujuzi wa Biblia katika Chuo Kikuu cha Stellenbosch katika Afrika ya Kusini, alitoa maelezo juu ya ulizo “Je! masomo ya ualimu wa dini yanachukua muda mwingi mno?” Katika Die Kerkbode (Februari 4, 1970, ukurasa wa 161), gazeti rasmi la kanisa la makanisa ya Kihollandi Yaliyotengemana katika Afrika ya Kusini, yeye aliandika:
“Mnamo masomo yote ya miaka saba, hakuna kujifunza Biblia kwa kweli wakati wo wote, kama awezavyo kushuhudia kila mhudumu. Matokeo ni kwamba ujuzi wa mhudumu kwa kawaida wa Biblia ya Kiafrikaans unaacha mengi ya kutamaniwa. Matokeo ni kwamba huduma yake inahasirika.”