Je! Uamini Utatu?
Ian Boyne, mwandikaji wa mambo ya dini kwa gazeti The Sunday Gleaner, Jamaica, West Indies, alizungumzia broshua iliyotolewa hivi karibuni na Mashahidi wa Yehova, akisema kwa sehemu hivi:
“Mashahidi wanastahili alama ya ‘A’ kwa kichapo hiki ambacho, ingawa kimeandikwa kwa usahili hivi kwamba tineja anaweza kukisoma, kimejawa na—bila kutia chumvi—manukuu kutoka kwa wanachuo na vyanzo vinavyoheshimika. . . . Kuchapishwa kwa Je! Uamini Utatu? ni tendo la akili sana la Mashahidi, na sasa hakuna mwamini wa Utatu—au mwamini wa uwili [mungu-wawili] aliye salama. Kijitabu hicho kinataja nukuu baada ya nukuu kutoka vyanzo vya kihistoria na kitheolojia kuonyesha kwamba fundisho la Utatu halitokani na Biblia. Kinanukuu Encyclopedia of Religion yenye mamlaka kuwa ikisema, ‘Wanatheolojia wanakubali kwamba Agano Jipya halina fundisho la wazi la Utatu.’”
Boyne aonelea hivi pia: “Ni jambo gumu sana kwa mwandikaji huyo wa mambo ya dini kuwazia ni kwa njia gani mshiriki wa kanisa aliye wa wastani—au hata wa juu—awezavyo kuzijibu hoja zenye nguvu na zenye amri zitolewazo na Mashahidi dhidi ya maoni ya kwamba Yesu ndiye Mungu.”
Ukipenda habari juu ya broshua hii, tafadhali jaza na upeleke kuponi inayoandama.
Ningependa kupokea habari ya broshua hii yenye kurasa 32, Je! Uamini Utatu?
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
Museo Bardini, Florence