Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 4/22 uku. 3
  • Tunaelekea Wapi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunaelekea Wapi?
  • Amkeni!—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Ulimwengu Huu Unaelekea Wapi?
    Amkeni!—2006
  • Ufundishaji Wenye Kusaidia kwa Ajili ya Nyakati Zetu Zenye Hatari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Hizi Ndizo Siku za Mwisho!
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Ni Nini Ishara ya “Siku za Mwisho”?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 4/22 uku. 3

Tunaelekea Wapi?

EBU wazia kwamba unasafiri kupitia eneo ambalo hujapata kuliona tena. Kufikia sasa ungepaswa kuwa umefikia mwisho wa safari yako, lakini ishara za barabara, majina ya miji, na alama za nchi hazilingani na zile ulizotazamia. ‘Niko wapi?’ wajiuliza. ‘Je, naelekea njia iliyo sawa?’

Ulimwengu wa leo uko katika hali sawa na hiyo. Mwanadamu yuko katika eneo asilolifahamu huku akitazama jamii ya watu ikidhoofika katika kiwango ambacho hakijapata kamwe kuonwa tena. Kukiwa na yale maendeleo yote katika sayansi na tekinolojia, ingeonekana kwamba kufikia wakati huu tungepaswa kuwa katika ulimwengu bora zaidi. Katika Great Ages of Man, mhariri Russell Bourne aonelea kwamba ni katika karne ya 20 tu kwamba “ile dhana ya zamani ya udugu wa kitufe imekuwa uwezekano wa kihalisi.”

Na bado, mwisho huo wa safari, “udugu wa kitufe,” umekosa kufikiwa. Zile alama zilizoahidiwa za usalama wa kiuchumi, chakula cha kutosha, afya iliyoboreshwa, na maisha ya familia yenye furaha hayapatikani popote. “Katika njia nyingi.” chaonelea kitabu Milestones of History, “maendeleo ya kisayansi yamehusianishwa moja kwa moja na uharibifu na ukatili.”

Ndiyo, mwanadamu leo amepotea katika eneo asilolifahamu, mbali sana na mkondo unaotakikana, mbali na amani na usalama ulioonekana mwanzoni mwa karne hii. Kwa hiyo, wengi leo wanaomba mwelekezo: “Tuliingiaje katika hali hii? Ulimwengu unaelekea wapi? Je, tunaishi katika siku za mwisho?”

Ili tujue mahali tulipo, lazima kwanza tuhakikishe tulipo sasa. Baadhi ya watu husema tuko mwanzoni mwa utaratibu wa ulimwengu mpya; wengine husema tuko ukingoni mwa uharibifu. Biblia, kama ramani ya barabara, yatusaidia kuona mahali hasa tulipo na tunakoelekea.

Unaposafiri, ni muhimu kutazama ishara zitakazotambulisha mahali ulipo. Sawa na hilo Biblia hufafanua mambo ya kutambulisha—hali za ulimwengu na mitazamo—ambayo ingeonyesha kipindi katika historia kinachoitwa “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1-5) Mtajo huu “siku za mwisho,” haurejezei kwenye mwisho wa mbingu na dunia halisi. Badala yake, humaanisha “umalizio wa mfumo wa mambo,” au “mwisho wa muhula,” kama tafsiri ya Biblia moja inavyosema.—Mathayo 24:3, New World Translation; Today’s English Version.

“Katika siku za mwisho,” akaandika mtume Mkristo Paulo, “nyakati za kipekee zilizo ngumu kushughulika nazo zitakuwa hapa.” (2 Timotheo 3:1, NW) Ni kweli huenda ionekane kwamba hili lingaliweza kuhusu vipindi vingine katika historia. Kwa kweli, kila muhula umekuwa na sehemu yayo ya kuteseka.

Kuna sababu gani basi, kuamini kwamba maneno haya yanataja hasa siku yetu?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

Tom Harley/Sipa Press

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki