“Kama Kuni Kwenye Moto”
HIVYO ndivyo Jennifer, msichana mwenye umri wa miaka 16 kutoka Oakland, California, Marekani, alivyofafanua magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! “Kwa kuendelea kuchochea bidii yangu kwa yaliyomo katika magazeti hayo, moyo wangu huwaka sana,” ndivyo anavyoeleza. “Namna makala hizo zilivyoandikwa,” asema, “ni wazi kwamba zinaandikwa ili kufunua ukweli wa mambo kwa wale wasiojua.”
Pia Jennifer aliandika kutoa shukrani kwa ajili ya “habari yote inayotetea uhalali wa Biblia.” Alisema: “Karibu kila mtu ninayezungumza naye hana uhakika katika Biblia. Uhakika wa kwamba habari hii yote inayothibitisha kwamba Biblia inastahili kuchunguzwa inachapishwa, hunijulisha kwamba habari hii haihitajiwi katika nchi yangu peke yake bali kila mahali.”
Hii ni kweli kabisa. Habari inayokazia thamani ya Biblia kwa wazi inahitajiwa ulimwenguni pote. Ndiyo sababu broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote imeandaliwa. Inajibu maswali kama vile: Je, Biblia inaweza kutumainiwa? Je, yaafikiana na sayansi? Je, ni kitabu kinachoweza kutumika kwa maisha ya kisasa?
Unaweza kupokea broshua hii yenye kurasa 32 kwa kujaza na kupeleka kuponi inayoandamana nayo ama kwa kutumia anwani iliyoonyeshwa kwenye kuponi ama kwa kutumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nipelekeeni nakala ya broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote.
Onyesha ni lugha ipi
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.