Amkeni! Lachochea Bango la Kupinga Uvutaji wa Sigareti
NA MLETA-HABARI WA AMKENI! KATIKA ITALIA
HIVI majuzi, katika jiji la Mortara kaskazini mwa Italia, Shirikisho la Italia la Kupambana na Kansa kwa kushirikiana na gazeti moja la huko lilipanga shindano la wanafunzi wa shule za sekondari la kuchora bango la kupinga uvutaji wa sigareti. Simona mwenye umri wa miaka kumi na minne, ambaye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova, alichunguza matoleo mbalimbali ya Amkeni! kuhusu hatari za tumbaku, na hasa toleo la Julai 8, 1989, na la Mei 22, 1995. Simona aandika hivi: “Nilipokuwa nikifanya utafiti, nilivutiwa na majalada ya matoleo haya. Nilichora fuvu lenye sigareti mdomoni jinsi nilivyoona kwenye Amkeni!, na kichwa chake cha jalada kilinisaidia kuteua shime ya bango langu.” Shime yake ilikuwa, “Uvutaji wa Sigareti—Huua Mamilioni ya Watu ili Kufanya Mamilioni.” Bango lake lilikuwa miongoni mwa mabango 250 yaliyokuwa shindanoni.
Ijapokuwa Simona alikuwa mchanga zaidi ya wanafunzi wengi kwenye shindano, alipewa zawadi ya kwanza, pamoja na msaada wa masomo wa dola 300. Simona aliandikia ofisi ya tawi ya Watch Tower Society ili kutoa shukrani kwa ajili ya majalada yenye matokeo ya Amkeni! yaliyomsaidia kuchora bango lake. Yeye hufurahia kusoma Amkeni! si kwa sababu tu ya majalada yake bali pia kwa sababu ya makala zake za wakati unaofaa na zenye habari inayotumika juu ya afya, matukio ya sasa, na matatizo yanayowakabili vijana. Akamilisha barua yake hivi: “Nyongeza: Endeleeni kuchapisha makala bora!”
Ikiwa ungependa kupokea habari zaidi juu ya mambo mengine yanayowaathiri Wakristo, tafadhali wasiliana na Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova lililo karibu nawe au peleka kuponi iliyopo hapa.
□ Nipelekeeni nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.