Je! Nafsi Ni Isiyoweza Kufa?
▸ Dini nyingi hufundisha kwamba kitu fulani ndani ya mtu—nafsi, roho, mzuka—ni kisichoweza kufa na huendelea kuishi baada ya kifo. Je! hilo ni kweli?
▸ Fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi lilianza namna gani?
▸ Namna gani fundisho hili lilikuja kuwa la msingi kwa dini nyingi za siku zetu?
▸ Kwa kweli nafsi ni nini?
▸ Kwa nini tunakufa?
▸ Jambo gani huifikia nafsi wakati wa kifo?
▸ Ni tumaini gani lililopo kwa wafu—na walio hai?
▸ Je! kile unachoamini kuhusu nafsi ni jambo la maana?
Majibu ya kweli na yenye kutosheleza ya maulizo haya yanapatikana katika kitabu cha zamani zaidi sana kilichopata kuandikwa. Unaalikwa kuyachunguza katika broshua hii.