Sala Iliyoongoza Mtu Akapata Kweli ya Mungu
◆ Katika Colombia mfanya kazi mmoja wa mkataba aliomba kwamba Mungu amtumie kwa njia fulani. Wakati mmoja wa mashahidi wa Yehova ambaye ni mmisionari, pamoja na mwenzake mwenye umri wa miaka kumi walipomtembelea, mfanya kazi huyu alisikiliza kwa makini. Kwa kuvutiwa na maarifa ya Maandiko ya mvulana huyo, mtu huyo akakubali kujifunza Biblia na mmisionari huyo. Muda mfupi baada ya hapo akatupilia mbali vitabu vyake vilivyohusu uchawi, akaacha kuvuta sigara kisha akazitupa sanamu baada ya kumweleza mke wake Biblia inavyosema juu ya ibada ya sanamu. Miezi kumi baada ya kuanza kujifunza Maandiko mtu huyo akabatizwa katika kusanyiko la wilaya la mashahidi wa Yehova.