Kweli ya Biblia Yaenea Kwa Njia ya Ajabu
● Katika kijiji kimoja cha Afrika magharibi, mmoja wa mashahidi wa Kikristo wa Yehova aliacha nakala ya Mnara wa Mlinzi katika jumba la dini isiyo ya Kikristo. Mwangalizi wa jumba hilo alitangazia wanavijiji baadaye kwamba, ‘Malaika wa Mungu ameleta ujumbe kijijini,’ kisha akaliinua gazeti hilo. Alijiongezea maneno yake mwenyewe akasema mtu ye yote aliyetaka baraka ya Mungu atoe mchango wa senti 80 au zaidi kwa kipande au ukurasa wa gazeti hilo.
Mwanamume mmoja mzee alinunua ukurasa mmoja. Aliyosoma yalitosha kumwamsha apendezwe na ujumbe wa Biblia. Karibuni akaanza kujifunza Maandiko na Mashahidi wa Yehova na kufanya maendeleo mazuri sana.