Kutafuta Kweli Kwathawabishwa
Katika Ireland watu wengine wamekuwa wakitafuta Mashahidi wa Yehova ili waulize juu ya kweli ya Biblia. Kwa mfano, katika kisa kimoja Shahidi mmoja aliangushia mwanamke mmoja kijitabu akakisoma na kumpa mumewe. Juma mbili baadaye, mwanamume huyu alikuja nyumbani kwa Shahidi huyu na kumwambia mke wake hivi: “Mume wako alimpa mke wangu kijitabu. Nimekisoma, na ndiyo kweli. Ningependa kuzungumza na mume wako. Nimekuwa nikimtafuta juma mbili hizi zilizopita.”
Mwanamume huyu alieleza kwamba anapendezwa sana na Biblia. Kwa kweli, alisema kwamba kwa kusoma Biblia ya Kikatoliki alikuwa amefahamu kwamba ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja. “Ninalotaka kujua ni hili,” akasema mwanamume huyu, “je! nina mahali katika ufalme huu?”
Mipango ilifanywa kwamba mume na mke hawa Mashahidi wamtembelee mtu huyu mwenye kuuliza habari pamoja na mke wake. Wakati wa ziara hiyo, mazungumzo marefu ya Biblia yalifanywa. Jumapili iliyofuata mume na mke hawa wenye kupendezwa walihudhuria na jamaa yao hotuba ya watu wote kwenye Jumba la Ufalme, na hii iliongoza kwenye funzo la kawaida la Biblia la nyumbani. Katika muda mfupi, jamaa hiyo yenye kutafuta kweli ilikuwa imekwisha kuondoa vitu vya ibada ya uongo katika nyumba yao na walikuwa wakifanya maendeleo mazuri ya kiroho.