Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 2/15 kur. 29-30
  • Kujiweza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujiweza
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 2/15 kur. 29-30

Kujiweza

HESABU fulani ya maneno ya lugha za asili yanatoa wazo la kuchunga, kuzuia au kudhibiti utu wa mtu, vitendo au usemi wake. (Mwanzo 43:31; Esta 5:10; Zaburi 119:101; Mithali 10:19; Yeremia 14:10; Matendo 24:25) Kuiweza ni ‘tunda la roho ya Mungu’ (Wagalatia 5:22, 23, NW) na Yehova amejizoeza tunda hilo nyakati zote, ingawa ana nguvu zisizo na mpaka. Badala ya kuchukua hatua ya mara hiyo dhidi ya wakosaji, yeye ameruhusu wakati upite ili wawe na fursa ya kugeuka kutoka njia zao mbaya na hivyo wapate upendeleo wake.​—Yeremia 18:7-10; 2 Petro 3:9.

Hata hivyo, ilipokwisha kuthibitishwa sana kwamba wale ambao walikuwa wamenyoshewa wakati wa kutubu hawakutaka kujifaidi na rehema yake, kwa kufaa Yehova aliacha kujizuia kufikiliza hukumu yake. Kisa kimoja kinahusu walioletea Yerusalemu ukiwa. Kwa kukosa kutambua kwamba Yehova aliwaruhusu wao waweze kuwadhibiti Waisraeli ili yeye awatie nidhamu kwa ukosefu wa uaminifu, waleta-ukiwa hao waliwatenda Waisraeli bila rehema na wakazidisha nidhamu hiyo kuliko vile hukumu ya Mungu ilivyokuwa imetaka. (Linganisha Isaya 47:6, 7; Zekaria 1:15.) Yehova alikuwa ametangulia kujua hilo na, kupitia nabii Isaya, alionyesha kwamba wakati ungekuja ambapo yeye hangezidi kujizuia kuadhibu waleta-ukiwa hao: “Mimi nimekuwa mnyamavu kwa wakati mrefu. Mimi niliendelea kuwa kimya. Mimi nilijizoeza kujiweza. Kama mwanamke anayezaa mimi nitaguna, nitahema, na kutweta wakati ule ule mmoja. Mimi nitateketeza milima na vilima, na majani yayo yote mimi nitayakausha kabisa.”​—Isaya 42:14, 15, NW.

Kristo Yesu pia alijizoeza kujiweza. Mtume Petro, alipokuwa akielekeza fikira za watumishi wa nyumbani kwenye uhitaji wa kujitiisha kwa wenyeji wao, aliandika hivi: “Kwa kweli, kwenye mwendo huu ninyi mliitwa, kwa sababu hata Kristo aliteseka kwa ajili ya ninyi, akiachia ninyi kiolezo ili ninyi mfuate kwa ukaribu hatua zake. . . . Wakati yeye alipokuwa akitukanwa, yeye hakurudisha kutukana. Wakati yeye alipokuwa akiteseka, yeye hakutisha, bali aliendelea kujikabidhi mwenyewe kwa yeye anayehukumu kwa uadilifu.”​—1 Petro 2:21-23, NW.

Katika “siku za mwisho” ukosefu wa kujiweza ungekuwa moja ya tabia zenye kuonyesha wale ambao hawangekuwa wakizoea Ukristo wa kweli. (2 Timotheo 3:1-7) Hata hivyo, kwa kuwa Wakristo wanapaswa kuwa waigaji wa Mungu na wa Mwana wake (1 Wakorintho 11:1; Waefeso 5:1, NW), inawapasa wao wajitahidi kusitawisha kujiweza katika mambo yote. (1 Wakorintho 9:25) Mtume Petro alitaarifu hivi: “Tieni uadilifu kwenye imani yenu, kwenye uadilifu wenu maarifa, kwenye maarifa yenu kujiweza, kwenye kujiweza kwenu uvumilivu, kwenye uvumilivu wenu kujitolea Mungu, kwenye kujitolea Mungu kwenu shauku ya kidugu, kwenye shauku yenu ya kidugu upendo. Kwa kuwa ikiwa mambo hayo yanakaa ndani yenu na kufurika, yatawazuieni msiwe ama wasiotenda ama wasiozaa matunda kwa habari ya maarifa sahihi ya Bwana yetu Yesu Kristo.”​—2 Petro 1:5-8, NW.

Sifa ya kujiweza inapasa hasa kuwa dhahiri miongoni mwa wale wanaotumikia wakiwa waangalizi katika makundi ya Kikristo. (Tito 1:8) Ili waangalizi wawe na matokeo mazuri ya kushughulikia matatizo ndani ya kundi, ni lazima wao wadumishe kujiweza katika neno na tendo. Mtume Paulo alishauri Timotheo hivi: “Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi. Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu; akiwaonya kwa upole wao washindanao naye.”​—2 Timotheo 2:23-25.

Kushindwa kujizoeza kujiweza katika hali fulani ile kunaweza kuleta sifa mbaya juu ya kumbukumbu ndefu ya utumishi wa uaminifu na kutumbukiza mtu ndani ya magumu ya aina zote. Kielezi cha jambo hilo ni tukio lililopata Mfalme Daudi. Ingawa alikuwa mshikamanifu kwa ibada ya kweli na alikuwa na upendo kwa kanuni za uadilifu za sheria ya Mungu (linganisha Zaburi 101), Daudi alifanya uzinzi pamoja na Bathsheba na jambo hilo likamwongoza kufanya Uria mume wake awekwe mahali fulani katika pigano ambapo ilielekea kuwa atakufa hakika. Tokeo ni kwamba, kwa miaka mingi baadaye, Daudi alipata pigo la magumu makali ndani ya jamaa yake. (2 Samweli 12:8-12) Kisa chake kinaonyesha pia hekima ya kuepuka hali ambazo zinaweza kuongoza mtu apoteze kujiweza. Ijapokuwa yeye angaliweza kuondoka juu ya dari la jumba lake la kifalme, ni dhahiri kwamba Daudi aliendelea kutazama Bathsheba alipokuwa akioga, na kwa hiyo akaja kuwa na harara kwa ajili yake.​—2 Samweli 11:2-4.

Vivyo hivyo, haingekuwa vizuri mtu mwenye ukosefu wa kujiweza abaki mseja na hali angeweza kuingia katika ndoa ya kuheshimika na hivyo ajihami mwenyewe dhidi ya kufanya uasherati. Katika habari hiyo, mtume Paulo aliandika hivi: “Ikiwa wao hawana kujiweza, acheni wao wafunge ndoa, kwa maana ni bora kufunga ndoa kuliko kuwa mwenye kuwaka harara.”​—1 Wakorintho 7:9, 32-38, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki