“Nimeacha kuamini kwamba hakuna Mungu! ”
“Mimi nilikutana na mwanamke mmoja wa kutoka Polandi ambaye ni profesa,” anaripoti mmisionari mmoja katika Senegal, Afrika. “Sisi tulikuwa na zungumzo refu, na nilijitahidi kujibu maswali yake mengi.” Profesa huyo alikataa kichapo fulani kilichokusudiwa kwa funzo la Biblia, akieleza hivi: “Mimi ni mtu anayeamini kwamba hakuna Mungu. Kitabu hicho hakinipendezi mimi hata kidogo.” Hata hivyo, mwanamke huyo alikikubali kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?
“Mimi niliporudi juma lililofuata,” mmisionari yule anaripoti, “mwanamke huyo aliniambia kwa msisimuko kwamba alikuwa amesoma kitabu kile kutoka jalada mpaka jalada. Nilipopendekeza kuchunguza kitabu Creation pamoja naye, yeye alijibu: ‘Lakini mimi sina uhitaji wa kujifunza kitabu hicho sasa! Nimekisoma chote, na kimebadili kabisa maoni yangu—nimeacha kuamini kwamba hakuna Mungu! Sasa mimi ningependa wewe ujifunze pamoja nami kitabu kile chekundu ulichonionyesha kwanza, pamoja na Biblia!’”
Je! wewe unajua mtu fulani ambaye anaamini kwamba hakuna Mungu au labda anayeuswali ukweli wa Biblia? Kwa sababu gani usipelekee mtu huyo nakala-zawadi ya Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Unaweza kufanya hivyo kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyo hapa chini, na utupelekee Kshs. 40.00 (Tshs. 150.00; RWF 250) tu pamoja na hati hiyo.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, nakala-zawadi ya kile kitabu chenye kurasa 256, Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?, na pia barua ya kueleza kwamba ni zawadi kutoka kwa ‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐ (jina lako). Mimi nawapelekea Kshs. 40.00 (Tshs. 150.00; RWF 250)