Maswali Kutoka kwa Wasomaji
■ Je! Yehova hutumia viini-macho au udanganyifu kuhusiana na watu, kutia na watumishi wake, kama vile Yeremia 4:10 na 20:7 yanavyoelekea kudokeza?
Sivyo, Muumba si mdanganyifu, mtunga hila, wala mjanja katika shughuli zake. Ingawa hivyo, yeye anaweza kutimiza na hutimiza penzi lake adilifu wanadamu wajapotarajia jambo lolote lile.
Tunaona upande mmoja wa jambo hilo kutokana na Yeremia 4:10, ambapo mnabii alisema hivi: “Aa, Bwana MUNGU [Yehova, NW] hakika umewadanganya sana watu hawa na Yerusalemu, ukisema, Mtakuwa na amani; lakini upanga umeingia katika nafsi za watu.”
Yehova alitumia Yeremia kutabiri afa lenye kujia taifa hilo asilililojidhania lilikuwa likimtumikia Yeye. (Yeremia 1:10, 15-19; 4:5-8; 5:20-30) Hata hivyo, walikuwako wengine wenye kudai kuwa ni wanabii. (Yeremia 4:9) Watu walisikia nini kwa hao wenye kuitwa wanabii eti? Mungu aliainisha jambo hilo hivi: “Manabii wanatabiri uongo . . . na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo.” —Yeremia 5:31; 20:6
Ingawa Yehova hakuwatuma hao wanabii bandia, yeye wala hakuwazuia wasieneze jumbe, kama vile: “Mtakuwa na amani” na, “Hamtapatwa na ubaya wo wote.” (Yeremia 23:16, 17, 25-28, 32) llikuwa lazima watu hao wachague—wakubali yale manabii ya kweli yaliyotolewa na Yeremia au wajiache waongozwe vibaya na wanabii bandia wa kujifanyiza wenyewe, kama Hanania na Shemaya. (Yeremia 28:1-4, 11; 29:30-32) Kwa kuwa Mungu hakuwazuilia wanabii hao wenye kuongoza watu vibaya, ingeweza kusemwa hivi juu yake: “Hakika umewadanganya sana watu hawa na Yerusalemu, ukisema, Mtakuwa na amani.”
Katika maana tofauti, Yeremia alipumbazwa. “Ee BWANA [Yehova, NW] umenihadaa, nami nimehadaika; wewe una nguvu kuliko mimi, ukashinda; nimekuwa kitu cha kuchekesha, mchana kutwa; kila mtu hunidhihaki.”—Yeremia 20:7.
Pashuri, kuhani mashuhuri, alimshambulia Yeremia peupe na kumtia katika mkatale. Kwa maoni ya kibinadamu, Yeremia angaliweza kuhisi kwamba alikuwa amefikia kikomo cha uvumilivu wake, kwamba hakuwa tena na imara ya kusonga mbele kwa kukabili ubaridi, kukataliwa, dhihaka, na jeuri ya kimwili. Lakini sivyo. Yehova alitumia imara Yake ili iwe dhidi ya mbetuko wa kibinadamu wa Yeremia, au iwe kinyume chao. Mungu alimpumbaza Yeremia katika jambo la kwamba Yeye alimtumia mwanadamu huyo asiyekamilika ili atimize mambo ambayo mnabii huyo asingaliweza kufanya kwa imara yake mwenyewe. Ingawa huenda ikawa Yeremia alipumbazwa au akashangazwa sana na jambo hilo, lilikuwa na kusudi jema: Wenye kumnyanyasa waliaibishwa, na ujumbe wa Mungu ukatolewa.—Yeremia 20:11.
Basi, yanapoeleweka kulingana na habari zinazozunguka, Yeremia 4:10 na 20:7 yanapatana na shauri lililokatwa na Elihu: “Mungu hatatenda mabaya, wala Mwenyezi hatapotosha hukumu.”—Ayubu 34:12.
■ Kwa nini Maombolezo 4:10 inarejezea akina mama waliokula watoto wao wenyewe kwa kuwasema kuwa “wanawake wenye huruma”?
Akieleza hali ya shida kubwa ya Wayahudi wakati wa mazingiwa ambayo Wababuloni walifanyia Yerusalemu katika 607 K.W.K., Yeremia aliandika hivi: “Mikono ya wanawake wenye huruma imewatokosa [imewachemsha] watoto wao wenyewe; walikuwa ndio chakula chao katika uharibifu wa binti ya watu wangu.”—Maombolezo 4:10.
Karne kadhaa kabla ya hapo, Musa alikuwa ameonya Waisraeli kwamba wakati ujao wao ungekuwa ama na “baraka” ama na “laana.” Wao wangeona shangwe ya kupata baraka wakishika amri za Mungu, lakini wangejiletea mteseko wakikataa njia zake adilifu. Moja la matokeo mabaya sana lilikuwa kwamba Waisraeli wangefikia hata kula watoto wao wenye hakuwatumawe. (Kumbukumbu 28:1, 11-15, 54, 55; 30:1; Walawi 26:3-5, 29) Hilo lilitukia kikweli baada ya Yehova kuliachilia taifa hilo lisilo na imani na lisilotii liingie katika mkono wa Wababuloni.
Katika Maombolezo 4:10 mnabii Yeremia aliutumia uhakika unaojulikana sana kwamba kiasili mama huwa na moyo mwororo, wenye huruma, na ni mwenye kuwapa himaya watoto wake. (1 Wafalme 3:26,27; 1 Wathesalonike 2:7) Hata hivyo, njaa kubwa iliyokuwa katika Yerusalemu uliozingiwa ilikuwa kali sana na kule kufa-njaa ilikotokeza kukawa na nguvu nyingi sana za kushurutisha hata akina mama ambao kwa kawaida wangekuwa na huruma wakatokosa na kula wazao wao kama binadamu-walabinadamu.—Linga Maombolezo 2:20.
Hali kama hiyo ilitukia baada ya Wayahudi kumkataa Mesiya, aliyekuwa ameonya juu ya mazingiwa ya Yerusalemu yaliyokuwa yakija. (Mathayo 23:37, 38; 24:15-19; Luka 21:20-24) Mwanahistoria Yosefo alieleza hivi juu ya moja la matukio yenye kuogofya sana ya mazingiwa katika 70 W.K.: “Wake walinyang’anya waume zao, watoto baba zao, nalililo baya zaidi ya yote—akina mama watoto wao wachanga, wakinyakua chakula kutoka ndani ya vinywa vyao hasa.” — The Jewish War, kilichotafsiriwa na G. A. Williamson, sura 19, ukurasa 291.
Kweli kweli, kuachilia mbali sheria na njia za Mungu sio mwendo wa hekima.