Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 7/1 uku. 32
  • ‘Fundisho la Msingi la Kiadili’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Fundisho la Msingi la Kiadili’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 7/1 uku. 32

‘Fundisho la Msingi la Kiadili’

Msichana wa miaka 14 kutoka Naijeria, Afrika ya Magharibi, anashukuru kwa kupokea fundisho hilo kutokana na kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako. Yeye anaandika hivi:

“Kitabu hiki ni mtungo wenye kusaidia sana, uliojaa ukweli, ulio mzuri ajabu na wenye kufurahisha sana. Kwa uhakika kitasaidia sana mtu yeyote aliye na mwelekeo wa kutaka kuongozwa apite yale madhambi mengi yenye kulemea watu maishani.

“Mimi nimetolea wanashule wenzangu na majirani kitabu hiki. Kila mmoja anayekisoma anapongeza vielezi vyenu vyenye ‘kuongezea maarifa’ ya kina kirefu na vichwa vya habari zilizozungumziwa katika kitabu chenyewe. Sisi tunaona kwamba mambo ya uhakika yaliyoonyeshwa katika kitabu hiki hayangewapa watu nuru ya elimu tu au kuwapa hekima na kanuni za mwenendo wenye kiasi kinachotakiwa ili kuwa na mafanikio, bali pia kingeweza kuwaandalia miongozo ya mwelekeo chanya vijana na watu wazima wanaotamani sana kuona shangwe ya kuwa na amani ya kweli ya akili na afya, na ambao wangetaka kujizoeza kujidhibiti na kuonyesha imara ya kutetea mambo yanayofaa. . . .

“Juu ya yote, kitabu hiki kina maelezo mengi sana na kimejaa sana fundisho la msingi la adili ya ngono ambalo huenda lisipatikane kwa wazazi au walimu walio wengi . . . Mimi naona sana ni laiti kitabu hiki kingejulishwa kwenye shule mbalimbali ili kitumiwe kwa masomo ya darasani kila siku, kwa lengo la kusimamisha imara mtindo-maisha ulio na amani nyingi zaidi, wenye kupendeka, wenye matunda mengi na umaana mwingi.”

Kupata Faida Zote za Ujana Wako kinajibu maswali kama, Kwa nini vijana wajifunze shuleni? Inawapasa wawe na maoni gani juu ya wazazi wao? Je! inawapasa kufanya ngono kabla ya ndoa? Je! inawapasa kunywa vileo? Pokea nakala kwa Kshs. 15/= tu kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyopo chini.

Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 192, Kupata Faida Zote za Ujana Wako. Mimi nawapelekea Kshs. 15/=

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki