Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 12/15 uku. 30
  • Je! Wewe Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kubaki Tukiwa Tumejipanga Kitengenezo Ili Tuokoke Kuingia Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Kufaidika Kutokana na “Mpatanishi Mmoja kati ya Mungu na Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 12/15 uku. 30

Je! Wewe Wakumbuka?

Je! wewe umefikiria kwa uangalifu matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, labda utaweza kukumbuka mambo yanayofuata:

◻ Paulo atumia mtajo “mpatanishi” katika maana gani arejezeapo habari za Yesu kwenye 1 Timotheo 2:5, 6?

Katika andiko hili, Paulo atumia neno la Kigiriki me·siʹtes la kusema “mpatanishi,” mtajo ambao una maana ya kisheria, kwa hiyo yeye hatumii neno hili katika ile maana pana yenye kutumiwa kwa kawaida katika lugha nyingi. Kwa sababu hiyo, Paulo hasemi kwamba Yesu ni Mpatanishi kati ya Mungu na aina ya binadamu yote. Bali, yeye anarejezea habari za Kristo akiwa Mpatanishi wa kisheria wa lile agano jipya, lililowawekea wafuasi wapakwa-mafuta wa Kristo msingi wa kushiriki naye katika Ufalme wake wa kimbingu. (2 Wakorintho 5:1,5: Waefeso 1:13, 14; Waebrania 8:7-13)—8/15, kurasa 30, 31.

◻ Kwenye Mathayo 25:34, NW, Yesu amaanisha nini asemapo hivi kwa wale walio kama kondoo: “Rithini ufalme uliotayarishwa kwa ajili ya nyinyi kuanzia kuwekwa misingi ya ulimwengu”?

Yesu hakumaanisha kwamba hawa walio kama kondoo watatawala pamoja naye mbinguni. Bali, kondoo hao watarithi makao ya kidunia ya Ufalme waliyotayarishiwa “kuanzia kuwekwa misingi ya ulimwengu” wa aina ya binadamu yenye kukomboleka. Kwa njia hii wao huwa watoto wa kidunia wa ‘Baba wa Milele’ wao, yule Mfalme, Kristo Yesu. (Isaya 9:6, 7)—9/1, ukurasa 20.

◻ Je! ingehitajiwa kabisa mabaki wapakwa-mafuta wawe hai duniani ili kukaribisha kurudi kwa wafufuliwa wenye imani waliokufa kabla ya 33 W.K.?

Sivyo, haingehitajiwa kabisa iwe hivyo. Wengi wa umati mkubwa watakaookoka dhiki kubwa wanazoezwa sasa kutunza madaraka ya kitengenezo. Kwa hiyo, wao wangeweza kutunza vizuri hali hiyo na kuzoeleza wafufuliwa mambo ya “dunia mpya” yenye kuwa chini ya “mbingu mpya.” (2 Petro 3:13, NW)—9/1, kurasa 20, 21.

◻ Ni mambo gani yenye kuhusika katika kupata ‘kuokolewa’? (Matendo 16:30, NW)

Takwa la msingi ni hili: “Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka.” (Matendo 16:31) Hii yahusisha ndani kutwaa maarifa sahihi ya makusudi ya Mungu na njia yake ya wokovu. Halafu ni lazima mtu ajizoeze imani katika Yesu Kristo kuwa ndiye Wakili Mkuu wa wokovu. (Yohana 3:16; Tito 2:14) Kufanya hivyo huweka Mkristo katika hali ya kuokolewa, lakini ni lazima sasa avumilie katika kufanya penzi la Mungu na kuendelea kushikamana na matakwa yote ya Mungu muda wote uliobaki wa maisha yake. Hapo tu ndipo yeye aweza kuokolewa kwenye uhai wa milele. (Mathayo 24:13)—9/15, ukurasa wa 7.

◻ Ni jinsi gani imani ya Noa ililaani ulimwengu vikali? (Waebrania 11:7)

Utii wa Noa na vitendo vyake vya uadilifu vilionyesha kwamba wengine mbali na yeye na jamaa yake wangaliweza kuokoka Gharika kama wangalikuwa na nia ya kubadili mtindo wa maisha yao. Ijapokuwako mibano kutokana na mnofu wake mwenyewe usiokamilika, ulimwengu wenye kumzunguka, na Ibilisi, Noa alithibitisha kwamba iliwezekana kuishi maisha yenye kufurahisha Mungu.—10/1, ukurasa wa 11.

◻ kwa nini yatupasa tulinde hata dhidi ya porojo nyepesi?

Huenda tukatamka neno lisilokusudiwa kuumiza mtu yeyote, lakini porojo hii yenye kuonekana kama isiyo na hatia huenda ikawa yenye kuumiza ikirudiwa, ikipambwa madoido, au ikipindwa, hivi kwamba yaharibu sifa ya mwenye kuongewa habari zake, ikimnyang’anya jina lake jema. (Mithali 20:19)—10/15, ukurasa wa 13.

◻ Ni faida gani ambazo huwapo wakati wenzi wa ndoa wameingwa nira yenye kusawazisha vizuri?

Mume na mke huwa katika hali ya kutiana moyo kuhusu kuabudu Mungu wao. Pia, wao waweza kutegemea Maandiko kwa mwongozo katika kutatua tofauti zao.—11/1, ukurasa wa 20.

◻ Amri Kumi zaweza kutusaidiaje leo?

Hizo hufunua maoni ya Yehova kuhusu mambo na hutumika kuwa vikumbusha vya wajibu wetu wa kupenda Mungu na jirani. (Mathayo 22:37-39; 2 Timotheo 3:16, 17)—11/15, kurasa 5, 6.

◻ Ni katika pindi gani tatu Mungu alinena huku Yesu na wanadamu wengine wakisikia?

Pindi ya kwanza ilikuwa wakati wa Yesu kubatizwa na Yohana Mbatizaji (Mathayo 3:17); ya pili ilikuwa wakati Yesu alipogeuzwa sura machoni pa Yakobo, Yohana, na Petro (Mathayo 17:5); na ya tatu ilikuwa katika Nisani 10, siku nne kabla ya kifo cha Yesu, wakati sauti ya Mungu iliposikiwa na umati wenye kusimama katika hekalu. (Yohana 12:28)—12/1, ukurasa 8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki