“Jitihada Ya Ainabinadamu Kutafuta-tafuta Mungu”
“Kitabu hiki kilikuwa cha kupendeza sana na chenye kuvuta sana fikira hivi kwamba sikuweza kukiweka chini,” aandika msomaji mmoja kutoka Houston, Texas, U.S.A. Alisema kwamba katika eneo lake kuna watu wa karibu kila dini yenye kuzungumzwa katika kitabu hicho, lakini akakiri hivi: “Mimi sikuelewa imani zao za msingi na jinsi ya kuwaelekeza kwenye Biblia kwa majibu. Kitabu hiki kimekuwa jibu kwa sala zangu.”
Mankind’s Search for God kina mazungumzo ya kina cha ndani yaliyofanyiwa utafiti kweli kweli juu ya dini kama vile Uhindu, Ubuddha, Utao, Ukonfyushasi, Ushinto, Uislamu, na Uyuda. Msomaji huyo wa kutoka Texas alionelea hivi: “Kitabu hiki chazungumzia imani za watu wengine kwa njia ya kiasi na yenye staha, huku kikiwatia moyo waendelee kumtafuta-tafuta Mungu wa kweli, Yehova. Na maneno yenyewe yatokezwa kwa njia yenye kugusa mtu binafsi kwa upendezi sana, ikikaribia kuwa ni kama mtu fulani ameketi karibu nawe mkiendelea na maongezi.”
Sisi tuna uhakika kwamba kile kitabu Mankind’s Search for God chenye kurasa 384 kitajibu mengi ya maswali yako. Ikiwa wewe wapendezwa na kupokea nakala, tafadhali jaza na upeleke kuponi iliyoambatishwa kwenye anwani iliyo chini.
Mimi ningependa kupokea kitabu chenye kurasa 384 na vielezi, Mankind’s Search for God.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Jumuiya ya Wakristo
Uislamu
Uhindu
Ukonfyushasi—
Utao—Ubuddha
Ubuddha
Ushinto
Uyuda
Dini za Kikabila