Azimio
Bila shaka hudhurio kwenye “Hakiya Kimungu” Mikusanyiko litakuwa limezidi lile la mwaka uliotangulia, ambapo watu 6,443,597 walikusanyika mahali 1,098 ulimwenguni pote, 93,822 wakibatizwa. Hotuba, “‘Kahaba’ Mwenye Sifa Mbaya Sana” iliyotolewa kwenye “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko yote, ilifuatwa na kutolewa kwa kitabu kilichojalidiwa chenye kurasa 320 na picha za kupendeza, Revelation—Its Grand Climax At Hand!, katika lugha zaidi ya 20. Msemaji aliambia wasikilizaji wake: “Tumieni kitabu kipya hiki vizuri katika mafunzo yenu ya kibinafsi na ya kundi. Kitumieni, pia, katika kutangazia ulimwengu kwamba Babuloni Mkubwa amehukumiwa maangamizi, kwamba mataifa sasa yanaelekeana uso kwa uso na Har–Magedoni, na kwamba ule upeo mtukufu utafikiwa katika utawala wenye uzuri mwingi mno wa Ufalme wa Yehova ulio mikononi mwa Kristo na bibi-arusi wake. Nyinyi mtakuwa wenye furaha katika kusikia na kushika mambo haya, ‘kwa maana wakati uliowekwa u karibu’!”—Ufunuo 1:3, NW.
Sisi, ambao tangu 1914 tumekuwa tukiishi katika “siku ya Bwana” na kwenye wakati huu wa hukumu ya kimungu, tunashangilia katika pendeleo lililo kuu kuliko mapendeleo yote, lile la kutumikia Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova chini ya Mfalme wa wafalme wake, Yesu Kristo. (Ufunuo 1:10) Sisi MASHAHIDI WA YEHOVA, tunashuhudiza kwamba:
(1) SISI TUNAKIRIHI (TUNACHUKIA KABISA) lile suto ambalo Babuloni Mkubwa, na hususa Jumuiya ya Wakristo, ametupa juu ya jina la yule Mungu mmoja wa kweli aliye hai, Yehova. Kwa upande wetu, SISI TUNAKUBALI KABISA kwa moyo mzima, kulingana na maneno ya Ufunuo 4:11, NW, kwamba: “Wewe wastahiki, Yehova, hata Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu.”
(2) SISI TUNAKIRIHI ushikamano wa Jumuiya ya Wakristo kwenye mafundisho ya Kibabuloni, hasa sana yale ya mungu mwenye umoja wa kiutatu, kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu, mateso ya milele katika moto wa mateso, pargatori yenye moto, na ibada ya mifano—kama vile Madonna na msalaba. Kwa kupatana na Ufunuo 22:18, 19, NW, SISI TUNAKAA KWA UTHABITI tukifuata kabisa Neno la Mungu lililoandikwa na yote yaliyomo.
(3) SISI TUNAKIRIHI falsafa na mazoea yenye kupinga Mungu, ambayo ni ya kawaida sana katika Jumuiya ya Wakristo, kama vile mageuzi, kutia damu mishipani, kutoa mimba, kusema uwongo, pupa, na ukosefu wa kufuata haki. Katika ibada yetu na njia yetu ya maisha, SISI TUTAHESHIMU Muumba wetu, Yehova Mungu, yule Mweza Yote, ambaye njia zake zinasimuliwa kwenye Ufunuo 15:3, NW, kuwa “za uadilifu na za kweli.”
(4) SISI TUNAKIRIHI kushindwa kwa Jumuiya ya Wakristo kutii ujumbe mbalimbali wa Yesu kwa yale makundi saba kwenye Ufunuo sura 2 na 3 katika mambo kama vile ufarakano, ibada ya sanamu, uasherati, uvutano wa Kiyezebeli, uvuguvugu, na ukosefu wa kulinda. Kwa upande wetu, SISITUTASIKIA NA KUTII mambo ambayo ile “roho husema kwa makundi.”
(5) SISI TUNAKIRIHI ule ukosefu wa adili na uendekevu ulio katika Jumuiya ya Wakristo na miongoni mwa viongozi wa kidini wake, na sisi tunakaribisha hukumu ya wazi ya Yehova iliyotaarifiwa kwenye Ufunuo 21:8, NW, kwamba wale wanaoendelea katika kinyaa chao—waasherati, waongo, na watu kama hao—wataharibiwa kabisa kabisa. SISI TUNAUNGA MKONO KWA MOYO MZIMA viwango vya Biblia kuhusu ngono, ndoa, na maisha ya jamaa.
(6) SISI TUNAKIRIHI ule umalaya wa kiroho wa karne nyingi wa viongozi wa kidini wa Babuloni Mkubwa katika kukubaliana kwa uwazi kabisa na watawala wa kilimwengu ili kupata nguvu, utajiri, na utawala wa kuonea watu wa kawaida. SISI TUNAAZIMIA kusaidia watu wenye moyo wa kufuata haki ili watii ule mwito wa malaika ulio kwenye Ufunuo 18:4, NW: “Ondokeni katika yeye, watu wangu.”
(7) SISI TUNAKIRIHI ile hatia ya damu iliyotungamana kutokana na uhai wa watu zaidi ya milioni 100 waliodhabihiwa vitani katika karne hii peke yayo, ambayo sana-sana inahesabiwa kuwa imesababishwa na uasherati wa yule kahaba mkubwa pamoja na serikali za kisiasa. SISI TUNASHANGILIA kwamba wakati uliowekwa u karibu wa Mungu kufikiliza adhabu ya kihukumu juu ya Babuloni Mkubwa, kama inavyotaarifiwa wazi kwenye Ufunuo 18:21-24.
Tukiwa Mashahidi wa Yehova, SISI TUNAIHESABU KUWA SHANGWE NA PENDELEO kutangazia ulimwengu kwamba katika 1914 “ufalme wa ulimwengu ulipata kuwa ufalme wa Bwana wetu [Yehova] na wa Kristo wake.” (Ufunuo 11:15, NW) SISI TUMEAZIMIA kusonga mbele bila hofu katika kujulisha hukumu za Yehova zilizotangazwa juu ya Babuloni Mkubwa na katika kuonya juu ya kukaribia sana kwa vita ya Mungu ya Har–Magedoni. SISI TUMEPIGA MOYO KONDE kuvumisha kwa sauti kubwa na “kwa kila taifa na kabila na ulimi na kikundi cha watu,” mwangwi wa zile habari njema kwamba “mbingu mpya na dunia mpya” ziko karibu mkononi ili kubariki aina ya binadamu iliyo tiifu. (Ufunuo 14:6; 21:1, NW) SISI TUNASHANGILIA kwamba kama tokeo la tangazo hili, mkutano mkubwa wa watu zaidi ya milioni tatu kutoka mataifa yote sasa umeungana kwa umoja pamoja nasi kuzunguka tufe letu. Pamoja na yule malaika anayeruka katikati ya mbingu, sisi sote tunatangaza hivi: “Hofuni Mungu na kumpa yeye utukufu, kwa sababu saa ya hukumu kwa yeye imewasili, na hivyo abuduni yule Mmoja ambaye alifanyiza mbingu na dunia na bahari na vibubujiko vya maji.”—Ufunuo 14:7, NW.
[Maswali ya Kujifunza “Azimio”]
1. Mashahidi wa Yehova wanashangilia katika nini sasa?
2. Kuhusiana na kila moja la mambo saba ya Azimio, taarifu (a) ni kitu gani Mashahidi wa Yehova wanakirihi na (b) ni jambo gani la mwelekeo chanya ambalo Mashahidi wanasema kwa uthabiti.
3. (a) Ni shangwe na pendeleo gani ambalo Mashahidi wa Yehova wanalo? (b) Ni nini azimio la Mashahidi? (c) Sisi tumepiga moyo konde kufanya nini pia? (d) Mashahidi wa Yehova wanashiriki katika ushangilio na tangazo gani?