Maelezo ya Chini
a Mtu ajuaye ana UKIMWI apaswa kufanya nini atakapo kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova na kubatizwa? Kwa kustahi hisia za wengine, huenda likawa jambo la hekima aombe ubatizo wa faragha, ingawa hakuna uthibitisho wa kudokeza kwamba UKIMWI umepitishwa katika vidimbwi vya kuogelea. Ingawa Wakristo wengi wa karne ya kwanza walibatizwa kwenye mikusanyano mikubwa ya watu wote, wengine walibatizwa katika mazingira ya faragha zaidi kwa sababu ya hali mbalimbali. (Matendo 2:38-41; 8:34-38; 9:17, 18) Njia nyingine ingekuwa kwamba yule mtaka kubatizwa mwenye UKIMWI abatizwe mwisho.