Maelezo ya Chini
b Miongozo ya 1995 hutumika kwa vikundi vingi vya umri lakini si vyote. “Kuna mwafaka wa jumla kwamba miongozo mipya ya uzito yaelekea haitumiki kwa watu walio na umri wa zaidi ya miaka 65,” asema Dakt. Robert M. Russell katika jarida JAMA la Juni 19, 1996. “Uzito wa kupita kiasi kidogo tu katika mtu mwenye umri mkubwa zaidi waweza hata kunufaisha kwa kuandaa hifadhi ya nishati kwa vipindi vya ugonjwa na kwa kusaidia kuhifadhi misuli na tishu za mifupa.”