Maelezo ya Chini
e Kuanzia 1919 hadi 1988, maombi na rufani katika jumla ya kesi 138 zilizohusu Mashahidi wa Yehova yalifanywa katika Mahakama Kuu Zaidi ya Marekani. Kesi 130 kati yazo zilipelekwa mahakamani na Mashahidi wa Yehova; 8, na washindani wao wa kisheria. Katika kesi 67 Mahakama Kuu Zaidi ilikataa kusikiliza tena kesi hizo kwa sababu, kama vile Mahakama ilivyoona jambo hilo wakati huo, hakukuwa na masuala ya maana ya kikatiba au kisheria ya taifa yaliyozushwa. Katika kesi 47 ambazo Mahakama ilisikiliza, maamuzi yaliwapendelea Mashahidi wa Yehova.